Jumapili, 8 Juni 2014

Friday, June 6, 2014

MKUU WA MKOA MBEYA ABBAS KANDORO AZINDUA HOTEL YA KISASA JIJINI MBEYA

PAZD HOTEL MBEYA

Mkuu wa mkoa Mbeya Abbas Kandoro akikata utepe kuzindua hotel ya Padz Hotel jijini Mbeya kushoto ni mkurugenzi wa Padz Hotel Patric D. Zambi



Baadhi ya wageni waalikwa wakishuhudia uzinduzi wa hoteli hiyo



Mkuu wa mkoa Mbeya Abbas Kandoro akiweka saini kitabu cha wageni kulia ni mkurugenzi wa hoteli hiyo Patric D. Zambi


PAZD HOTEL MBEYA

Thursday, June 5, 2014

IMETOKEA ASUBUHI YA LEO: MTOTO AFARIKI DUNIA HAPO HAPO BAADA YA CHUMBA ALICHOKUWEMO KUTEKETEA KWA MOTO ILOMBA JIJINI MBEYA.

Askari wa jeshi la Polisi akichukua mwili wa marehemu baada ya ajali.
 Baadhi ya majirani wakishuhudia uokoaji wa ajali ya moto.
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Ilomba, Amir Kitululu akizungumza jambo akiwa katika eneo la tukio.
 Baadhi ya vitu vikiwa vimenusurika kutokana na ajali hiyo.
Mama mzazi wa Marehemu, Winfrida Sokon akiwa anashangaa  bila kuamini kilichotokea baada ya moto kumwangamiza mwanaye.

MTOTO mwenye umri wa miaka Mitatu na nusu aliyefahamika kwa jina la Rehema Patrick amefariki dunia baada ya chumba alichokuwa amelala kuteketea kwa moto.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa limetokea leo asaubuhi majira ya saa moja asubuhi huko katika Mtaa na kata ya Ilomba jijini Mbeya.
Amesema chanzo cha moto huo hakijafahamika ambapo mtoto huyo ambaye ni marehemu alikuwa amelala wakati mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Winfrida Sokon (30), alikuwa ameenda kuchota maji huku naye baba yake akiwa safarini.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Mtaa, Amiri Kilulu, amesema Mama huyo ni mgeni amehamia jana tu akiwa na watoto wawili ambao ni Tukulamba Mwakyami(4) pamoja na marehemu, lakini huyo mkubwa  ndiye aliyegundua moto huo.
Amesema mtoto huyo baada ya kugundua moto huo alimfuata mama yake alikokuwa akichota maji lakini walipofika walikuta mtoto ameshafariki dunia ambapo majirani walijaribu kuuzima bila mafanikio.
Jeshi la polisi lilifika eneo la tukio na kuondoka na marehemu kwa ajili ya uchunguzi zaidi huku majirani nao wakichangishana fedha kwa ajili ya kusaidia mazishi kutokana na ugeni wa mwanamke huyo.

NA MBEYA YETU

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni